KARIBU

Tuesday, February 14, 2012

Mtoto wa sumari ataka kumrithi baba yake

MBIO za kuwania ubunge wa Arumeru Mashariki zimeanza na tayari jana wananchama wawili wa CCM walijitokeza kuchukua fomu kuwania tiketi ya kupeperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi huo.
Katibu wa CCM wa Wilaya ya Arumeru mkoani Arusha, Edson Lihweuli amewataja waliochukua fomu zilizoanza kutolewa jana kuwa ni Williamu Sarakikya (38) na Sioi
Sumari.
Kwa mujibu wa Lihweuli, Sarakikya ambaye ni mkazi wa Nkoaranga ndiye aliyekuwa mwanachama wa kwanza kuchukua fomu hiyo na kufuatiwa na Sioi ambaye ni mkazi wa Kijiji cha Akheri. Sioi ni mtoto wa kwanza wa marehemu Sumari; mbunge aliyepita aliyepita katika Jimbo hilo la Arumeru Mashariki.
Tambo za wagombea
Mara baada ya kuchukua fomu, Sarakikya alisema katika uchaguzi uliopita alikosa nafasi hiyo ya kuteuliwa kwa kuwa alikuwa mgenikatika siasa. Sarakikya alisema katika muda huo alijifunza mengi kuhusu siasa na sasa amejipanga kikamilifu kuwania nafasi hiyo na hatafanya makosa.
Naye Sioi alisema amechukua fomu za kuwania ubunge, ili ashiriki kupunguza ama kumaliza changamoto zilizopo ndani ya jimbo hilo. Sumari alisema yeye ni mkazi wa jimbo hilo na ameshatembelea matawi yote na kujua changamoto hizo ila kwa sasa hawezi kuzitaja mpaka muda ukifika atazitaja na namna gani atashirikiana na wana CCM na wasio wana CCM kuzipatia ufumbuzi.
Mgombea wa CCM
Wakati huo huo Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC) iliyomaliza kikao chake Dodoma juzi, imetoa ratiba ya mchakato wa kumpata mgombea wa chama hicho atakaye peperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi huo.
Kwa mujibu wa ratiba hiyo ya NEC iliyokuwa ikiongozwa na Mwenyekiti wa chama hicho, Rais Jakaya Kikwete, mgombea wa chama hicho atatangazwa rasmi Februari 27, mwaka huu na Kamati Kuu ya chama hicho.
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye alisema jana kuwa mwisho wa kuzirudisha fomu zilizoanza kutolewa jana ni Februari18, mwaka huu. Alisema Februari 20,mwaka huu Mkutano Mkuu wa jimbo hilo utaitishwa ili kupiga kura za maoni, tofauti na ilivyozoeleka kura hizo kupigwa kwenye matawi.
“Mabadiliko haya ni kwa uchaguzi huu mdogo tu kwa sababu hatuna muda wa kuzunguka kwenye matawi yetu yote ya jimbo hilo,” alisema Nape. Alisema Februari 21, mwaka huu Kamati ya Siasa ya Wilaya itajadili wagombea na kutoa mapendekezo yake kwa Kamati ya Siasa ya Mkoa na Februari 24 mwaka huu Kamati hiyo ya mkoa itajadili na kutoa mapendekezo yake kwa Kamati Kuu ya CCM.
Kwa mujibu wa ratiba hiyo, Februari 27 mwaka huu Kamati Kuu ya chamahicho itateua na kumtangaza rasmi mgombea wa chama hicho katika jimbo hilo. Uchaguzi katika jimbo hilo unafanyika baada ya aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Jeremeih Sumari kufariki dunia mapema mwezi uliopita kwa ugonjwa wa saratani ya ubongo.
Uchaguzi wa madiwani
NEC pia ilitoa ratiba ya uchaguzi wa madiwani katika kata nane za Tanzania Bara ambazo pia wanachama walianza kuchukua fomu jana lakini mwisho wa kuzirejesha utakuwa Februari 16, mwaka huu. Nape alisema kuanzia Februari 17 hadi 21, mwaka huu itakuwa ni muda wa kampeni za uchaguzi kwenye matawi hayo na Februari 22 kutafanyika mikutano mikuu ya matawi ya kupiga kura za maoni.
Kwa mujibu wa ratiba hiyo, Februari 25 mwaka huu kamati za siasa za wilaya zitajadili wagomea na kutoa mapendekezo yao kwa kamati za siasa za mikoa ambazo nazo zitawajadili wagombea hao na kutoa mapendekezo Februari 27 na halmashauri kuu za mikoa zitateua wagombea Februari 29, mwaka huu.
Taarifa zingine NEC
Pamoja na hayo, Nape alisema NEC pia ilipokea maelezo kutoka serikalini kuhusu kumalizika kwa mgogoro wa madaktari nchini na mchakato wa upatikanaji wa Katiba mpya. “Wajumbe wameitaka Serikali kuhakikisha inachukua hatua haraka za kumaliza kabisa mgogoro huo ili usirejee tena na kuitaka ijijengee utamaduni wa kumaliza migogoro kama hiyo mapema kabla ya kuleta madhara makubwa kwa wananchi,” alisema.
Alisema mkutano huo pia ulijadili suala la chama hicho kuanzisha Kamati ya Maadili ambapo mjadala mkali uliibuka wa kutaka ama kamati hiyo iingizwe kwenye katibaya chama hicho au la.
Alisema katika kukamilisha mambo zaidi ya 20 ya mabadiliko ya chama hicho ikiwemo kujivua gamba, tayariwameanza kupata mafanikio hasa katika eneo la kutaka chama hicho kujiendesha chenyewe bila kutegema ruzuku. Kwa sasa kwa mujibu wa Nape, mikoa mitatu ikwemo Mwanza, Arusha na Dar es Salaam inajiendesha yenyewe

Washindi wa tuzo za grammy

Tuzo za Grammy 2011 zenye Category 78 zimetolewa nchini Marekani usiku wa kuamkia leo ambapo ulikua ni usiku pia wa kumkumbuka Whitney Houston, kabla mzigo hujaanza nataka nikupitishe kwanza kwa baadhi ya picha za waliostua kwenye REDCARPET.
rapper Nicki Minaj akiwa na mtu asiefahamika ambae alivaa kama Papa.
huyu mrembo aliwasili na Adam Levine
Mwimbaji Adele ndio ameongoza kwa waimbaji wa kike waliochukua tuzo nyingi usiku huo ambapo amechukua tuzo sita.
RECORD OF THE YEAR: Rolling In The Deep (ADELE)
ALBUM OF THE YEAR: 21 -(ADELE)
SONG OF THE YEAR: Rolling In The Deep (ADELE)
BEST NEW ARTIST: Bon Iver
BEST POP SOLO PERFOMANCE: Someone Like You (ADELE)
Best Pop Duo/Group Performance: Body And Soul Tony Bennett & Amy Winehouse
Best Pop Vocal Album: 21 (ADELE)
Best Traditional Pop Vocal Album: Duets II Tony Bennett & Various Artists
Best Rock Performance: Walk Foo Fighters
Best Rock Song: Walk Foo Fighters
Best Rock Album: Wasting Light Foo Fighters
Best R&B Performance: Is This Love Corinne Bailey Rae
Best Traditional R&B Performance: Fool For You Cee Lo Green & Melanie Fiona
Best R&B Song: Fool For You Cee Lo Green, Melanie Hallim, Jack Splash, songwriters (Cee Lo Green & Melanie Fiona)
Best R&B Album: F.A.M.E. - Chris Brown
Best Rap Performance: Otis (Jay-Z & Kanye West)
Best Rap/Sung Collaboration: All Of The Lights (Kanye West, Rihanna, Kid Cudi & Fergie)
Best Rap Song: All Of The Lights - (Kanye West, Rihanna, Kid Cudi & Fergie) ambapo zilizokua
zinashindania hiyo tuzo ni Black And Yellow, I Need A Doctor, Look At Me Now, Otis
na The Show Goes On ya Lupe Fiasco.
Best Rap Album: My Beautiful Dark Twisted Fantasy (Kanye West)
Best Country Solo Performance: Mean(Taylor Swift)
Best Country Song: Mean - Taylor Swift, songwriter (Taylor Swift)
Best Gospel/Contemporary Christian Music Performance: Jesus - Le'Andria Johnso
Best Gospel Song: Hello Fear - Kirk Franklin, songwriter (Kirk Franklin)
Best Gospel Album: Hello Fear - Kirk Franklin
Hapo chini ni VIDEO ya Perfomance ya Rihanna kwenye tuzo hizo……
Washindi wengine wa Grammy mwaka huu ni Best American Album: Ramble At The Ryman – Levon Helm
Best Reggae Album: Revelation Pt 1: The Root Of Life - Stephen Marley
Best World Music Album: Tassili - Tinariwen
Best Comedy Album: Hilarious -Louis C.K.
Best Historical Album: Band On The Run - (Paul McCartney Archive Collection - Deluxe Edition)
Paul McCartney, compilation producer; Sam Okell & Steve Rooke, mastering engineers
(Paul McCartney & Wings)
Best Short Form Music Video: Rolling In The Deep -Adele
Producer Of The Year, Non-Classical: Paul Epworth ambae amehusika kutengeneza hits kama
*. Call It What You Want (Foster The People) (T)

Thursday, February 2, 2012

Ajali yaua wanafunzi saba korogwe girls

Vifo hivyo vimetokea baada ya mwanafunzi aitwaye KIBIBI MMASA kuingia ndani ya gari la kaka yake lenye namba T489 AGJ na kuanza kulichezea,wakati akiwa ndani ya gari mara akaweka gia ya kurudi nyuma na kuanza kurudi nyuma kwakasi ya 120 km kwa saa na kuwaparamia wanafunzi waliokuwa katika kusherekea mahafali hayo na kusababisha vifo hivyo.

Fomu za big brother zatoka

Fomu za ushiriki wa shindano la BIG BROTHER AFRICA zimetoka leo, ambapo tayari mpaka saa tano asubuhi watanzania zaidi ya 15 walikua tayari wamejitokeza kuchukua hizo fomu ambazo zinatolewa bure.
haya ni baadhi ya maswali yaliyopo kwenye fomu.
historia yako, lugha ya nyumbani ni ipi? na ni lugha zipi nyingine unazoongea?
Relation status yako? kilichowahi kukufurahisha sana kwenye maisha yako, kilichowahi kukuhuzunisha sana?
ni kitu gani kibaya sana ulishawahi kukifanya? elezea ndani ya maneno 50, zitaje tabia zako zinazokera wengine, wewe ni mdini? eleza msimamo wako wa kisiasa.
Elezea uhusiano wako na mtu uliechagua kuingia nae, eleza kwa nini unataka kuingia BBA, elezea uhusiano wako na familia, elezea aina ya maisha unayoishi, Afya yako, unavuta sigara? kama ndio, ngapi kwa siku?
maswali haya yafuatayo, hayatakufanya ushindwe au uweze kuingia BBA!!!!!! una matatizo sugu ya kiafya? utakubali kupima HIV? una matatizo ya akili?
BBA ya mwaka huu itaanza May ambapo washiriki kutoka nchi 15 za Afrika watashiriki

pata nguo kali kutoka izzo biz clasic wear

wiki hii itakua ni nzuri sana kwa msanii anaeiwakilisha Mbeya, mzee wa kuongea na mshua, Izzo B atazindua duka lake jipya jijini mbeya maeneo ya soweto stand ya kuelekea mjini."duka langu linaitwa
IZZO BIZNESS CLASSIC WEAR alisema Izzo"..Hongera zake za kutosha, keep it locked

boti zagongana mwanza, 30 wafariki

0digg



share

Boti zagongana, 30 wanusurika kifo!

ZAIDI ya watu 30 wamenusurika kufa kwa kuzama majini, baada ya boti walizokuwa wakisafiria kugongana katika Ziwa Victoria, Wilaya ya Musoma Vijijini Mkoani Mara; imethibitishiwa.
Imeelezwa kwamba ajali hiyo imetokea hii leo majira ya saa 3:15 asubuhi katika eneo Rethi, ambapo boti moja iliyokuwa ikisafirisha abiria kutoka Mwigobero mjini Musoma kwenda Kisiwa cha Rukuba kugongana uso kwa uso na boti nyingine ya wavuvi, jambo lililosababisha taharuki kubwa.Taarifa kutoka mjini Musoma zinaeleza kwamba, boti ya abiria ilikuwa na watu 28 na mizigo nyingi, huku boti ya wavuvi ikiwa imebeba wavuvi wawili, na kwamba watu wote waliokolewa.
Kwa mujibu wa taarifa hizo zilizothibitishwa pia na Kamanda wa Polisi Mkoani Mara, Robert Boaz (RPC), zinasema kwamba, baada ya boti hizo kugongana iliharibika na kusababisha maji mengi kuanza kujaa ndani, ambapo abiria wote walipatwa na hofu kubwa.
“Ni kweli ajali ipo na watu kama 30 hivi nusura wafe kwa kuzama majini. Watu hawa walikuwa kwenye boti ndani ya Ziwa Victoria, lakini boti hizo hazikuwa na vifaa vya kujiokolea.
“Hii ajali imetokea asubuhi leo, na abiri walikanyagana baada ya ajali kutokea. Kila mmoja alitaka ajiokoe mwenyewe kabla ya kuokolewa”, alisema mashuhuda mmoja wa ajali hiyo, Fikiri Aloyce Malenge.
Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo, Kamanda wa Polisi Mkoani Mara, Robert Boaz alisema: “Kweli hii ajali imetokea leo, majira ya saa 3 hivi asubuhi. Na katika ajali hii boti moja ilikuwa na abiria 28, lakini ile ya wavuvi ilikuwa na watu wawili?
“Hizi boti ya wavuvi na ile ya abiria zimegongana uso kwa uso. Lakini watu wote walifanikiwa kuhamia kwenye boti ya wavuvi na hakuna aliyefariki dunia hata mmoja”, alisema Kamanda wa Polisi Mkoa huo wa Mara, Boaz.
Alisema, chanzo cha ajali bado hakijajulikana na kwamba jeshi lake linaendelea na uchunguzi kuhusiana na ajali hiyo mbaya, na kwamba hakuna mtu yeyote aliyekamatwa kuhusiana na tukio hilo?
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoani Mara, Boaz, abiria wote walipatiwa huduma ya kwanza papo hapo na kuruhusiwa kuendelea na majukumu yao ya kawaida.
Habari hii imeandikwa na Sitta Tumma – Mwanza

mkenya aingia uchi uwanjani

Jamaa mmoja mwenye asili ya kenya aliingia uwanjani akiwa uchi wa mnyama kwenye mechi kati ya England na Argentina kwenye michuano ya Rugby World Cup - 2011 inayofanyika nchini New Zealand .

Inasemekana jamaa ni mzaliwa wa Kenya ana miaka 23 na alikua hajavaa kitu zaidi ya kuchora uso wake,na alikatiza kwenye uwanja wa Otago na kuonekana na mamilioni ya watazamaji wa television duniani,baadaye alikamatwa na wana usalama na huenda akakabiliwa na kifungo che miezi 3 jela au faini ya dola 5,000.
Wachambuzi wa mambo wanadai kuwa jamaa huyo aliamua kufanya hivyo ili kujizolea umaaru duniani.

wabunge waigomea serikali

WABUNGE wamekataa kupitisha azimio la Serikali la kupunguza ushuru wa maji ya chupa kutoka sh. 69/- hadi Sh. 12/- kwa chupa kwa kuwa punguzo hilo halitamnufaisha mwananchi wa kawaida.

Wabunge wametoa msimamo huo leo mchana baada ya Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo, kumaliza kujibu hoja za wabunge waliochangia hoja ya Azimio la Bunge la Kuridhia Marekebisho ya Jedwali la Nne la Sheria ya Ushuru wa Bidhaa sura ya 147 iliyowasilishwa bungeni leo asubuhi.

Baada ya Mkulo kumaliza kujibu hoja hizo na kuwaomba wabunge wapitishe azimio hilo, Mbunge wa Buchosa, Dk. Charles Tizeba (CCM), aliomba mwongozo na kutaka hoja hiyo iondolewe kwa kuwa haina manufaa kwa mlaji wa mwisho.

Dk. Tizeba amesema, punguzo hilo halitamnufaisha mwananchi kwa kuwa halitekelezeki kwenye soko la rejareja hivyo iondolewe, ijumuishwe kwenye bajeti ya Serikali ya mwaka ujao wa fedha.

Amesema, punguzo hilo litawanufaisha wenye viwanda na akamkariri Waziri Mkulo kuwa amewasilisha hoja hiyo baada ya kushawishiwa.

Baada ya Mbunge huyo kutoa hoja yake, Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai, alisema, Dk. Tizeba hakutumia kanuni sahihi kuwasilisha hoja yake lakini kanuni za Bunge zinatoa fursa kwake kuwahoji wabunge kama wanaunga mkono hoja ya msingi au la.

Aliwahoji wabunge, wengi wakaikataa hoja ya Serikali. “Wasioafiki wameshinda, kwa hiyo itabidi tujipange upya wakati mwingine kadri hali itakavyoruhusu” amesema Ndugai.

Kabla ya wabunge kugoma kupitisha azimo hilo, wabunge walitoa mawazo tofauti kuhusu punguzo hilo wakiwemo waliounga mkono na kuna waliopinga.

Mbunge wa Viti Maalum, Leticia Nyerere (Chadema), aliipongeza Serikali kwa kuwa sikivu na kuwasilisha azimio la punguzo hilo la ushuru wa maji ya chupa litakaloikosesha serikali mapato ya takribani shilingi bilioni 7.7/-

Amesema , umefika wakati kwa Serikali kuwa sikivu na ichukue mawazo bila kujali anayetoa anatoka chama gani. “Tunaruhusu tofauti ambazo hazileti mantiki katika maendeleo ya Taifa letu” amesema Mbunge huyo.

Dk. Tizeba ameipongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kuvilinda viwanda vya ndani lakini akamtaka Waziri Mkulo alieleze Bunge kwa nini alikaidi ushauri wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Fedha na Uchumi kuhusu suala hilo.

Mbunge amesema bungeni kuwa, wajumbe wa kamati hiyo ni Watanzania na wana mapenzi na nchi yao hivyo Mkulo aseme limepata hasara kiasi gani kwa kukaidi ushauri wa kamati hiyo.
“Niseme tu kwamba huu ni mwenendo mzuri” amesema Dk. Tizeba na akaongeza kwamba, hana uhakika kama kuwasilisha azimio hilo sasa ni usikivu .

Mkulo ameomba radhi kwa niaba ya Serikali kwa kuchelewa kuwasilisha azimio hilo, na kwamba, haikuwa dhamira ya Serikali au uzembe ila hali halisi. Amesema, punguzo hilo la ushuru halitakuwa na athari yoyote kwa uchumi wa nchi na litawasaidia wananchi kwa kiasi fulani.

Mbunge wa Kisarawe, Selemani Jafo (CCM) amesema, ni aibu kuagiza maji kutoka nje ya nchi, na amedai kuwa hakuna dhamira ya kutosha kulinda viwanda vya ndani.

Amependekeza kuongezwa kwa ushuru kwa maji yanayoagizwa kutoka nje ya nchi na akadai kuwa mwenendo wa kuagiza bidhaa kutoka nje ukiendelea fedha ya Tanzania haitakuwa imara.

“Leo hii tunapozungumzia maji tunazungumzia uchumi wa nchi” amesema Mbunge huyo na kupinga kupunguza matumizi mengine ya Serikali.

Mkulo amesema, maji ya chupa yanayotoka nje ni asilimia 20 ya maji yanayotumiwa nchini na kwamba, kupunguza matumizi ya Serikali si jambo jipya kwa kuwa lilishazungumzwa hata kwenye bajeti ya mwaka huu wa fedha 2011/ 2012.

Mbunge wa Viti Maalum, Zarina Madabida (CCM) ameipongeza Serikali kwa kulinda viwanda vya ndani lakini amehoji punguzo hilo linamsaidia nani.

Madabida amesema, punguzo hilo ni dogo sana kwa mlaji wa mwisho, hivyo amependekeza ushuru wa bidhaa kutoka nje uongezwe na ikiwezekana zizuiwe kuingizwa nchini.

Amesema, kupunguza ushuru kutoka sh. 69/- hadi sh. 12/- kwa chupa ya maji ni sawa na kupunguza sh. 57 tu kwa mlaji wa mwisho hivyo hakutamletea nafuu yoyote hivyo amekataa kuunga mkono hoja hiyo.

Mbunge wa Kalenga, William Mgimwa (CCM), amesema, kitendo cha serikali kuendelea kutoza ushuru wa sh. 69/- kwa chupa ya maji inayozalishwa nchini ilikuwa ni kukaidi ushauri uliotolewa na Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi.

Amemtaka Waziri wa Fedha atafute namna ya kufidia punguzo hilo na aseme athari za uamuzi huo.

Mbunge wa Lushoto, Henry Shekifu (CCM), ameitaka Wizara ya Fedha itafute vyanzo vingine vya mapato na iongeze ushuru kwa maji yanayotoka nje ya nchi.

Amemtaka Waziri wa Fedha atafute vyanzo vingine vya mapato badala ya kukata matumizi serikalini kwa kuwa kutaifanya Serikali ishindwe kujiendesha na kushinda pia kuwadhibiti watendaji.

 
     

okwi ainogesha simba

ImageSIMBA jana ilizidi kujikita kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu baada ya kuifunga JKT Oljoro mabao 2-0 katika mechi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Hata hivyo iliichukua Simba mpaka dakika ya 60 kupata bao hilo lililofungwa na Emmanuel Okwi aliyeingia uwanjani kuchukua nafasi ya Davies Kago. Okwi alifunga bao hilo kwa kumalizia
kazi ya Uhuru Selemani aliyekuwa akiwatoka mabeki wa Oljoro toka upande wa kushoto.

Okwi aliwainua tena mashabiki wa Simba vitini katika dakika ya 83 baada ya kufunga bao la pili kwa kazi nzuri ya Uhuru aliyemtengea mpira kabla ya kuujaza wavuni. Matokeo hayo yanaifanya Simba kuendelea kutesa kileleni ikiwa na pointi 34 huku mpinzani wake wa jadi Yanga ikiwa na pointi 31.

Simba ilicheza mechi hiyo pungufu karibu muda wote wa kipindi cha pili baada ya
mwamuzi Isihaka Shirikisho kumpa Haruna Moshi 'Boban' kadi nyekundu kwa kumchezea
rafu Omari Mtaki katika dakika ya 43.

Baada ya kadi hiyo wachezaji wa Simba walimzonga mwamuzi hali iliyolazimu mchezo kusimama kwa muda, kwa ujumla katika mechi hiyo, hasa kipindi cha kwanza wachezaji wa pande zote mbili walichezeana kibabe.

Kabla ya kadi hiyo, Boban, Mwinyi Kazimoto na chipukizi Jonas Gerald walishirikiana vema katikati na kutengeneza nafasi kadhaa ambazo zilizuiwa na ngome ya Oljoro chini ya Mtaki.

Dakika ya 71 nusura kipa wa Simba Juma Kaseja aiponze timu yake kutokana na mbwembwe zake alipokuwa akiuchezea mpira ukawahiwa na washambuliaji wa Oljoro shukrani kwa beki Kelvin Yondani aliyewahi kuukoa mpira huo uliokuwa ukielekea wavuni.

MASANJA KATIKA MZIKI WA INJILI

Mchekeshaji wa ORIJINO KOMEDI Masanja Mkandamizaji alipokua Dodoma akifanya video ya moja kati ya nyimbo zake za Gospel.
hii picha kaiweka kwenye page yake ya fB alafu akaandika: PIPOOO!!! Hebu iwekee maneno picha hii... Ni kama nasemaje vilee??

ggggg

Did you mean: www.millarddays .com Official – Millard Ayo Website VIDEO: FID Q – IELEWE MITAA. Posted: 2nd February 2012 by MillardAyo in Uncategorized Tags: fid q … millardayo.com/ HUYU NDIO BIBI ANAERAP NA KUIMBA! « Official – Millard Ayo ... Jan 20, 2012 … huyu ndio bibi ambae ana rap na kuimba, maajabu yake ameyaonyesha kwenye XXL ya CLOUDS FM … millardayo.com/ yes kijana kazi nzur - Bio « Official – Millard Ayo Website 2010 Official – Millard Ayo Website.All Rights Reserved. Greyzed Theme created by The Forge Web Creations. millardayo.com/ WANIGERIA WASIMAMISHA MGOMOKWA MUDA! « Official ... Official – Millard Ayo Website. the TZA…. news ni biz! … Posted: 13th January 2012 by MillardAyo in Uncategorized … millardayo.com/ millard ayo | Facebook millard ayo | Facebook. … To interact with...

dfgdfhg

rthjfdty

 
Design by Free WordPress Themes | Bloggerized by Lasantha - Premium Blogger Themes | Facebook Themes